ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Thursday, November 23, 2017

ZAIDI YA RAIA 800 KUTOKA CONGO WAKIMBILIA KIGOMA KUHOFIA AMANI

 Mkuu   wa   Mkoa   wa   Kigoma   Brig.   Jen.   Emannuel   Maganga   (mwenye   kofia) akikagua makazi ya raia waomba hifadhi kutoka Congo DRC  katika kituo cha Kigadye Wilayani Kasulu.
  Baadhi ya raia kutoka Jamuri ya Kidemokrasia ya Congo DCR wakifuatilia ujio wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kigoma ilipowasili kukagua  kituo cha Kigadye Wilayani Kasulu.

   Baadhi ya raia kutoka Jamuri ya Kidemokrasia ya Congo DCR wakifuatilia ujio wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Kigoma ilipowasili kukagua  kituo cha Kigadye Wilayani Kasulu.
 
    Mmoja wa waomba hifadhi akieleza mbele ya Kamati ya Ulinzi ya Mkoa sababu zilizo wafanya wakimbilie Tanzania

    Mwakilishi wa Shirika la kuhudumia wakimbizi  UNHCR Kigoma(mwenye kofia ya bluu)   akimwelezea Mkuu wa Mkoa wa Kigoma hali ya kituo cha kupokelea Wakimbizi Kigadye.

ZAIDI YA RAIA 800 KUTO CONGO WAKIMBILIA KIGOMA KUHOFIA AMANI
    Takribani   raia  800   kutoka   Jamhuri   ya   Kidemokrasia   ya   Kongo,   wamekimbilia
    Nchini Tanzania kuomba hifadhi ya ukimbizi katika kijiji cha Kigadye Wilayani
    Kasulu, Mkoani Kigoma wakihofia machafuko.

    Raia hao ambao wengi wao wanatoka maeneo ya Fizi na misisi Kivu kusini mwa
    Congo wamedai kuwa Vikosi na wapiganaji wa maimai nchi Congo na vikundi
    mbalimbali vya waasi vinavyoendelea kupigana nchini vimewatia hofu na  hivyo
    kuanza kukimbia nchini Tanzania kuomba hifadhi ya ukimbizi.

    Wakizungumza   mbele   ya   kamati   ya   ulinzi   na   usalama   ya   Mkoa   wa   Kigoma
    iliyotembelea katika kituo cha kupokelea waomba hifadhi kijiji cha Kigadye raia
    hao walisema sababu iliyowafanya kukimbilia Tanzania ni hofu ya usalama wa
    maisha yao kutokana na mapigano yanayoendelea kati ya vikundi vya waasi na
    Serikali iliyopo madarakani.

    Mkuu   wa   Mkoa   wa   Kigoma   Brigedia   Jenerali   (mst.)   Emannuel   Maganga
    akiongoza kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa amesema tayari Mkoa umefika
    kuwaona   raia   hao   na   wanafana   jitihada   za   kuhakikishah   wanapatiwa   huduma
    muimu   za   kibinadamu   zinaboresha  katika   eneo   hilo wakati   kamati   ya  taifa   ya
    kusikiliza maombi ya ukimbizi inajiadaa kuwasikiiza raia hao.

    Kutokakana na wimbi kubwa hilo huduma za kibinadamu ikiwemo chakula, malazi
    zinahitajika haraka ili kuwahudumia raia hao ambao wengi wao ni kinamama na
    watoto.                  

    Baadhi   ya   raia   waliokimbilia   nchini   Tanzaia   wamedai   kuwa   kutokana   na
    kuahirishwa Uchaguzi Mkuu uliopaswa kufanika Desemba, 2017 dalili za kuzuka
    kwa mzozo wa mapigano uenda ukawaathiri amani nchini Congowa,  Vyama vya
    upinzanu   vimeanza   kuonesha   dalili   za   kupinga   kusitishwa   kwa   uchaguzi,
    wamehofia amani.

    Kituo cha kigadye wilayani kasulu, huenda kikashindwa kimili idadi kubwa ya raia
    wa Congo wanaoendelea kfika kituoni hapo kwa madai ya kukimbia vita nchini
    mwao. Kusini mwa Congo kumekuwa na matukio ya hivi karibuni mashambulio
    ya mara kwa mara yanayosabisha hofu ya machafuko kwa wananchi.


 
    Habari na Picha zimeandaliwa na.
    Gabriel Ng’honoli
    Afisa Habari
    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kigoma


Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.