ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, August 24, 2016

MWADUI YATOKA VICHWA CHINI CCM KIRUMBA, YABAMIZWA 1-0 NA TOTO AFRICANS.

Kikosi cha Toto African.
TIMU ya Toto African ya Mwanza imeanza vyema Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kushinda bao 1-0 dhidi ya Mwadui FC ya Shinyanga.

Mfungaji wa bao la pekee kwa Toto African alikuwa, Waziri Junior dakika ya 36 aliyemshinda mbio beki wa Mwadui na kufumua shuti maridhawa lililomshinda kipa wa Mwadui Shahban Kadri na kutinga nyavuni. 


Huo unakuwa mwanzo mzuri kwa kocha Rogasian Kaijage aliyechukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa kocha wa timu hiyo John Tegete aliyeondolewa baada ya msimu uliopita kumalizika – na mwanzo mbaya wa kocha wa Mwadui, mwenye tambo na maneno mengi Jamhuri Kihwelo ‘Julio’.

Kikosi cha Mwadui Fc.

Mabadiliko ya Toto African ndani ya ungwe ya kipindi cha pili, Frank Sekule (9) anaingia badala ya Hamad Mbumba anayetoka (25), pembeni kushoto anaonekana kocha wa Mwadui Fc Jamhuri Kihwelo.


Hadi mwisho wa mchezo mashabiki walishuhudia Mwadui Fc wakitoka vichwa chini mara baada ya kukomelewa bao 1-0 dhidi ya Toto African ya Mwanza.

Tupe maoni yako

0 comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.