ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Friday, December 18, 2015

AJALI MBAYA YA BASI YAUA NA KUJERUHI VIBAYA IRINGA.

Watu 12 wafariki dunia na wengine 22 wakijeruhiwa vibaya baada ya basi la kampuni ya New Force kugongana na lori la mizigo mkoani Iringa. 

 Lori likiwa limeacha njia mara baada ya kugongana na basi hilo la abiria la kampuni ya New Force katika jali mbaya iliyotokea hii leo mkoani Iringa. 


 Hali ilivyo mara baada ya ajali ya basi la kampuni ya New Force kugongana na lori la mizigo mkoani Iringa, ambapo jumla ya watu 12 wamepoteza maisha na 22 wamejeruhiwa.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa Peter Kakamba amethibitisha watu 12 kupoteza maisha katika ajali hiyo. Wanane ni wanae na wanne ni wanawake.

Abiria 28 wamejeruhiwa wakiwemo madereva wa basi na roli na hali zao siyo nzuri.


Ajali hiyo imetokea majira ya saa nane alasili ambapo basi la Kampuni ya New Force aina ya Youtong lenye namba za usajili T483CTF likitoka Tunduma kwenda Dar limegongana na lori aina ya Scania lenye namba T616DEF katika kijiji cha Mahenge wilaya ya Kilolo mkao wa Iringa katika barabara kuu ya Dar - Mbeya.


Majeruhi wamelazwa hospitali ya wilaya ya Ilula, kilomita 45kutoka Iringa mjini.

BOMOABOMOA YAENDELEA KULIZA WENGI KINONDONI.

Vilio ,simanzi na majonzi vyaendelea kufuatia zoezi la bomoabomoa kuingia siku ya pili katika eneo la mto msimbazi wilayani Kinondoni.

NEW Official Music Video Best Nasso - Rumba

Hii ni video mpya ya Best Nasso inaitwa Rumba, Audio ya wimbo imetayarishwa na Chief Maker kutoka studio za Chief Music na video ikiwa imetayarishwa na kuongozwa na Kenny Ukiyz. 

HARAKATI ENDELEVU ZA KIKUNDI CHA “BUKOBA MPYA PROJECT” ZOEZI LA KUTOKOMEZA MAZALIA YA MBU KATA ZA MANISPAA YA MJI BUKOBA


HARAKATI ENDELEVU ZA KIKUNDI CHA “BUKOBA MPYA PROJECT”

ZOEZI LA KUTOKOMEZA MAZALIA YA MBU KATA ZA MANISPAA YA MJI BUKOBA

Ndugu Wadau,

“Bukoba Mpya Project” ni zao la harakati endelevu chini ya Bukoba Wadau Media katika kuchangia kuhamasisha Wanabukoba wa ndani na nje ya Tanzania kushiriki katika kuinua hali ya mji na maisha ya wakazi wa Bukoba.  Wanachama wa harakati hizi ni waamini wa itikadi ya UMOJA na MAENDELEO. Mpaka sasa jumla ya wanachama wasioupungua 50 kutoka ndani na nje ya Bukoba na Tanzania kwa ujumla wanashiriki harakati hizi.

Wakiongozwa na imani kwamba “maendeleo yanaletwa na mimi”, Wana Bukoba Mpya wamepanga kuanza jitihada ya kupambana na Malaria kwa kutokomeza mazalia ya mbu kwenye maeneo yote ya Manispaa ya Bukoba. Jitihada hii itatekelezwa kwa zoezi la kupulizia dawa za kuua mazalia ya mbu kwenye Kata zote 14 za Manispaa ya Bukoba. Zoezi litaanzia na Kata za Greenbelt  (Kahororo,Buhembe, Kitendaguro ,Ijuganyundo,Nyanga,Kibeta na Nshambya) mara tu baada ya siku kuu kuisha kisha litaendelea kwenye kata zingine zote kadri ratiba itakavyotolewa.

Kila mmoja anayeguswa na athari za mbu na anavutiwa na jitihada hii anaalikwa kushiriki kwa njia moja au nyingine. Unaweza kufanya hivyo kwa:

·         Kuthibitisha kushiriki moja kwa moja kwenye zoezi tarehe na mahali litakapofanyika
·         Kwa kuhamasisha ndugu na jamaa zako wafike kushiriki (hii ni kwa walio mbali na nje ya Tanzania)
·         Kwa kuchangia pesa, madawa na vifaa vya zoezi (orodha ya vifaa na utaratibu utapatiwa)

Viongozi, Watendaji na Wananchi kwa ujumla waombwa kutoa ushirikiano na kushiriki kwa kadri wanavyoweza pale zoezi hili litakapofanyika katika maeneo yao.

Kwa mawasiliano na maelezo zaidi juu ya jinsi ya kushiriki wasiliana nasi kwa njia zifuatazo:
Mob: 0784 505045 / 0768 397241 /0713 883020 /0754 505043.


Imetolewa na:
Kitengo cha Uhamasishaji Jamii
Bukoba Wadau Media


MAKUBWA YAIBUKA DHIDI YA BARABARA 6 ZA MANISPAA YA KINONDONI.

Taarifa mpya ya uchunguzi yabainisha upotevu wa kiasi cha shilingi bilioni 5.7 katika ujenzi wa barabara 6 za Manispaa ya Kinondoni.

DROO YA TATU YA PROMOSHENI YA "Jaza Mafuta na Ushinde" ya GAPCO YAFANYIKA JIJINI DAR.

Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam wa kampuni ya GAPCO Tanzania, Jane Mwita (kati) akibonyeza kitufe kwenye kompyuta kuwatafuta washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya "Jaza Mafuta na Ushinde" inayoendeshwa na Kampuni hiyo kwa Wateja wake wa jijini Dar es Salaam,ambapo zaidi ya wateja 25 huibuka kidedea kila wiki. Kulia anaeshuhudia ni Mkaguzi wa michezo ya kubahatisha nchini, Chiku Saleh na Kushoto ni Meneja Masoko wa GAPCO Tanzania, Caroline Kakwezi.
2015-12-18 0:58 GMT+03:00 Othman Michuzi :
Meneja wa Kanda ya Dar es Salaam wa kampuni ya GAPCO Tanzania, Jane Mwita (kati) akibonyeza kitufe kwenye kompyuta kuwatafuta washindi wa droo ya tatu ya promosheni ya "Jaza Mafuta na Ushinde" inayoendeshwa na Kampuni hiyo kwa Wateja wake wa jijini Dar es Salaam,ambapo zaidi ya wateja 20 huibuka kidedea kila wiki. Kulia anaeshuhudia ni Mkaguzi wa michezo ya kubahatisha nchini, Chiku Saleh na Kushoto ni Meneja Masoko wa GAPCO Tanzania, Caroline Kakwezi.

KICHUPA CHA 'UTANIPENDA' CHA DIAMOND NYUMA YA PAZIA.

Diamond platinumz (4)Nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwa  kasimama mbele ya magari aliyoyatumia katika video yake mpya ya Utanipenda.
Diamond platinumz (10)Staa wa Bongo, Jacqueline Wolper, akiongea jambo na Diamond.
Diamond platinumz (7)Gari ya Wolper katika video hiyo  ikimmwagia maji Diamond.
Diamond platinumz (5)
Diamond akiangalia vipande vya video hivyo kabla ya kuendelea kushuti.
Diamond platinumz (8)Diamond akiangalia Magazeti Pendwa baada ya kupata matatizo,  nayo hayakuwa nyuma kuandika.
Diamond platinumz (1)Diamond akipiga kinanda huku akimuimbia mpenzi wake Zari.
Diamond platinumz (12)Mama yake Diamond, Sanura Kasim (kushoto) akifukuzwa na mlinzi baada ya kwenda kuomba msaada kwa JK.
Diamond platinumz (11)Diamond akiongea jambo.
Diamond platinumz (2)Diamond akiwa kapozi na mpenzi wake Zari.
Sasa hivi kwenye ulimwengu wa muziki, gumzo ni ngoma aliyoitoa Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ inayokwenda kwa jina la Utanipenda.

Ni ngoma kali ambayo itatambulishwa kwa mara ya kwanza ndani ya Ukumbi wa Kimataifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala jijini Dar.

Mbali na utambulisho wa ngoma hii ambayo itapigwa live kwa kutumia vyombo, nyimbo nyingine ambazo Diamond atazipiga siku hiyo ni pamoja na Mdogomdogo, Nasema Nawe, Nana na nyinginezo zinazobamba huku akiwa na madansa wake kutoka Wasafi Classic Baby (WCB).

Itakuwa ni siku ya Krismasi (Ijumaaa ijayo) ambayo msanii huyo ameahidi kufanya mambo makubwa akisindikizwa na mkali wa nyimbo za Singeli, Msaga Sumu pamoja na wacheza dansi hatari Afrika Mashariki, Wakali Dancers na wasanii wengine kibao.

Burudani yote hiyo ambayo imedhaminiwa na huduma kutoka kampuni ya simu Tanzania, Airtel Money utaipata kwa kiingilio cha shilingi 15,000 tu getini na wale watakaohitaji huduma ya VIP watalipia shilingi 30,000.

Katika kuelekea kwenye shoo hiyo, Showbiz ilifanikiwa kunasa baadhi ya picha za nyuma ya pazia ‘behind the scene’ wakati kichupa cha wimbo huo kikiandaliwa.

Video hiyo ni mkono wa yuleyule mkali wa vichupa kutoa Sauzi anayekwenda kwa jina la God Father. Hajakosea! Amefanya bonge la kazi na hata mashabiki ni mashahidi kwamba wimbo ni mkali na kideo chenyewe ni ‘kitamu’.

Maneno mengi siyo ishu, kwenye hili picha zinaongea zaidi hivyo pitisha macho kwenye baadhi ya picha hizo ili upate uhondo!
Kwani kuna mtu kaibiwa?
Imeandaliwa na Andrew Carlos/GPL

Thursday, December 17, 2015

HARUSI YA DAVID NA VANESSA ILIVYOFANA JIJINI MWANZA.

Mara baada ya kufunga ndoa takatifu katika kanisa la AICT Makongoro na kisha kufuatiwa na sherehe ya kufana baadaye jioni katika ukumbi wa Gold Crest Hotel Mwanza, David na Vanessa walifika katika ufukwe wa Bismark Rock jijini Mwanza kwaajili ya kupata picha za kumbukumbu.
"Wewe ni wangu" alisikika David akimwambia Vanessa.
Toka eneo moja hadi jingine maharusi hawa alitumia usafiri huu.
Maharusi na wapambe wao.
Bi Vanessa.
Mtoko wa jioni....
Maharusi na ndugu zake David.
Wow....
Bi. Vanessa.
Check time na Mr. David Simba.
Ukumbi wa harusi.
Bi. Vanessa.
The colour.
Jinsi walivyokutana.
Ze Usafiri.
Kisha mtoto akaingia kingi kwa David.....!!!
Harusini maharusi walikuwa wa kwanza katika kutoa ukarimu kwa waalikwa kuwapatia chakula.
Mikato ya Bwana harusi akiwa na mpambe wake..
Flowers na Bi harusi.