ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

ZIMA KILA KITU ILA WASHA JEMBE FM 93.7 MWANZA

Wednesday, April 24, 2024

MSIFANYE KAMPENI KINYEMELA KABLA YA MUDA WAKE -KATIBU CCM KIBAHA MJI


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA 


Katibu wa Chama cha mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kibaha mjini Issack Kalleiya amekemea vikali tabia ya baadhi ya wanachama kuanza kufanya kampeni za chini chini na kutangaza nia kwa ajili ya kuwania nafasi mbali mbali za uongozi kabla ya muda kitu ambacho ni kinyume kabisa na taratibu za chama.

Katibu huyo ameyasema hayo wakati wa ziara yake ya kikazi kata ya kongowe yenye lengo la kuweza kuzungumza na wanachama wa CCM ikiwa pamoja na kuimarisha uhai wa chama kuanzia ngazi za matawi,mashina pamoja na Kata husika.

Kalleiya ambaye katika ziara yake aliambatana na viongozi mbali mbali wa chama alisema kuwa lengo kubwa ni kuweka misingi imara ya kukijenga chama kuanzia katika ngazi za chini hadi ngazi za juu.

Aliongeza kuwa anashangazwa kuona baadhi ya wanachama kwenda kinyume na taratibu zilizowekwa kwa kuanza kutangaza nia kinyemela ya kuwania katika nafasi mbali mbali za uongozi.
"Nipo katika ziara yangu yemye lengo la kuona namna ya kusimamia mwenendo mzima kwa wanachama ili waweze kuimarisha uhai mzuri kuanzia katika ngazi za matawi,mashina na ngazi nyingine,"

"Kitu kingine ambacho nakemea vikali ni hili suala la baadhi ya wanachama kuanza kufanya kampeni za chini chini za kutaka kuwania nafasi mbali mbali za chama kwa kweli hii sio sahii kwani muda wake ni bado,"alisisitiza Katibu Kalleiya.

Aliongeza katika chama cha mapinduzi kuna miongozo ambayo ipo wazi katika mambo ya uchaguzi hivyo ni lazima kila mwanachama anapaswa kuwaacha viongozi waliopo madarakani wamalize muda wao bila kuvunjiwa heshima.

Katibu huyo pia alliwahimiza wanachama wote wa ccm kuhakikisha kwamba wanajisajili kwa mfumo mpya wa njia ua kieletroniki ili waweze kutambulika kwa urahisi.

Alisema kwamba kwa sasa chama kinaendelea kuwahimiza wanachama wake kufanya uchaguzi mbali mbali ili kuweza kujaza nafasi nafasi ambazo bado zimeachwa wazi.
Katika aliongeza kuwa chama cha mapinduzi kikiimarisha kuanzia katika ngazi za chini kitaweza kuleta matokeo chanya na kuibuka na ushindi katika uchaguzi  wa serikali za 
 mitaa ambao unatarajiwa kufanyika mwaka huu pamoja na uchaguzi mkuu mwaka 2025.

Saturday, April 20, 2024

LEO BARABARA ZOTE ZA JIJI LA DAR ES SA;AAM KUELEKEA MWENGE - TANGAZO ANOINTED MINISTRY 2024

 𝗘𝘄𝗲 𝗺𝘁𝘂 𝘄𝗮 𝗠𝘂𝗻𝗴𝘂 𝗵𝗶𝗶 𝗶𝗻𝗮𝗸𝘂𝗵𝘂𝘀𝘂 𝗻𝗶 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝗹𝗲𝗼 𝘁𝗮𝗿𝗲𝗵𝗲 𝟮𝟬𝘁𝗵 𝗔𝗽𝗿𝗶𝗹 𝟮𝟬𝟮𝟰 𝗗𝗮𝗿 𝗲𝘀 𝗦𝗮𝗹𝗮𝗮𝗺 𝗶𝘁𝗮𝘁𝗶𝗸𝗶𝘀𝗶𝗸𝗮....

. . . . . #JEMBEGOSPLE

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI PWANI LAWAFUNDA WANANCHI JUU YA KUJIKINGA NA MAFURIKO NA MAAFA

 


NA VICTOR MASANGU,PWANI 


Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani Katika kukabiliana na majanga mbali mbali yakiwemo ya  moto na mafuriko ya mvua imetoa elimu kwa zaidi ya wananchi 72862 juu ya kujikinga na majanga pindi yanapotokea.

Hayo yamebainishwa na Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani Mrakibu mwandamizi Jenifa Shirima wakati akizungumzia mipango na mikakati waliyojiwekea katika kupambana na majanga ya aina tofauti.

Kamanda Shirima alisema kwamba lengo lao kubwa ni kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi juu  ya kujikinga na majanga mbali mbali hasa katika kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha.

"Sisi kama jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani tumeendelea kutoa elimu kwa wananchi wetu na kwamba tumeshafanikiwa kwa kuwafikia wananchi wapatao 72862 na kimsingi bado tunaendelea,"

"Katika zoezi ili la kutoa elimu kwa wananchi wetu wa Mkoa wa Pwani tangu Julai 2023 hadi kufikia mwezi Aprili mwaka huu tumepiga hatua kubwa ya kutoa elimu hiyo ambayo idadi yake ni 72862,"alisema Kamanda Shirima.

Kadhika Shirima alifafanua kuwa pamoja na kutoa elimu hiyo pia wameweza kupata fursa ya kutoa elimu juu ya tahadhari dhidi ya mafuriko ambayo yanatokea kutokana na mvua.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo alibainisha kuwa wameshapita kutoa elimu katika mikusanyiko ya watu mbali mbali ikiwa sambamba na kuanzisha sehemu maalumu za Fire club ambazo zitasaidia katika kupambana na majanga.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo aliwasisitiza wananchi ambao wamefanikiwa kupatiwa mafunzo hayo kuendelea kuyatumia vizuri ili yaweze kuwa msaada mkubwa katika jamii inayowazunguka.

Friday, April 19, 2024

RFO PWANI-TUMEFANIKIWA KUOKOA WANANCHI 2397 MAFURIKO YA RUFIJI NA KIBITI

 


NA VICTOR MASANGU,PWANI 


Kamanda wa Jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani  Mrakibu mwandamizi Jenifa Shirima amesema kwamba hadi kufikia leo Aprili 19 wamefanikiwa kuokoa wananchi wapatao 2397 kutoka Wilaya za Rufiji na Kibiti mkoani Pwani ambao walikubwa na mafuriko ya mvua na makazi yao kuzingirwa na maji.

Akizungumza katika mahojiano maalumu kuhusiana na mwenendo mzima wa hali halisi ilivyo kwa sasa  Kamanda huyo alibainisha hali ya makambi ambayo yametengwa kwa ajili ya wahanga yapo salama.






Kamanda huyo alisema kwamba kutokana na mvua ambazo zinaendelea kunyesha katika maeneo mbali mbali ziliweza kusababisha baadhi ya wananchi kukosa  makazi yao na hivyo serikali kuamua kuwatafutia maeneo mengine ambayo ni salama zaidi.

Alisema kwamba wameweza kufanikisha zoezi la uokoaji wa wananchi hao kwa kushirikiana bega kwa bega na vyombo vingine vya ulinzi na usalama kwa lengo la kuwatoa wananchi katika maeneo yaliyozingirwa na maji.

"Kwa sasa wananchi wote ambao tumeweza kufanikiwa kuwaokoa wameifadhiwa na serikali katika makambi maalumu ambayo yapo katika Wilaya ya Rufiji na Kibiti na yapo katika hali salama ", alisema Kamanda Shirima.

Kadhalika alibainisha kuwa tangu zoezi hilo lilipoanza mnano tarehe 9 machi mwaka huu la kuwavusha watu katika maeneo mbali mbali ambayo wanayooshi ili kuwapeleka maeneo salama.

Pia aliongeza kuwa zoezi rasmi kwa ajili ya uokoaji wa watu ambao wanaishi katika maeneo mengine ya mbali lilianza kufanyika kuanzia Aprili 7 mwaka huu hadi kufikia leo hii kufikia idadi ya watu waliookolewa kufikia 2397.

Katika hatua nyingine Kamanda huyo alitoa rai kwa wananchi wa Wilaya ya Kibiti pamoja na Rufiji kuhakikisha wanaondoka katika maeneo hatarishi na kukubali kwenda katika maeneo salama ambayo yametengwa na serikali.

Nao baadhi ya wananchi wa   Wilaya ya Kibiti na Rufiji wameishukuru kwa dhati serikali pamoja na wadau mbali mbali wa maendeleo kwa kuwapatia misaada ya kibinadamu kutokana na kupata mafuriko hayo.

Pia hawakusita kumshukuru Mkuu wa Mkoa wa Pwani pamoja na Kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa Pwani kwa kujituma kwa kipindi chote katika kuwasaidia na  kuokoa maisha yao.

WAZIRI JERRY SILAA KUONGOZA KLINIKI YA ARDHI TANGA

 

Na Oscar Assenga,TANGA

WAZIRI wa Ardhi,Nyumba na Mendeleo ya Makazi Jerry Silaa anatarajiwa kuongoza Kliniki ya Ardhi kwa mkoa wa Tanga itakayofanyika kuanzia Aprili 22 mpaka 28 mwaka huu ikifanyika kwenye maeneo mawili Kijiji cha Miaka 21 Chumbageni Tanga na Korogwe.

Akizungumza na waandishi wa habari leo,Kamishna Msaidizi wa Ardhi mkoa wa Tanga Tumaini Gwakisa alisema zoezi hilo litafanyika kwenye maeneo mawili ambapo litaanzia Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi wa Mkoa wa Tanga eneo la Kijiji cha miaka 21 Chumbageni kuanzia Aprili 22 mpaka 25 mwaka huu.

Alisema baada ya kumaliza kwa Tanga wataelekea wilayani Korogwe ambapo litafanyika kuanzia Aprili 26 mpaka 28 mwaka hu na uendeshwaji wa program hiyo utasimaiwa na itaongozwa na Waziri wa Ardhi Jerry Silaa akiwa na wataalamu wa Wizara hiyo.

“Nichukue nafasi hii kwaalika wananchi wote wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kupata huduma mbalimbali za sekta ya ardhi katika maeneo ambayo kliniki hiyo itafanyika kwani kutakuwa na utatuzi wa migogoro ya ardhi ambapo Waziri atasikiliza kero mbalimbali za Migogoro hiyo”Alisema

Alisema pia kutakuwa na utolewaji wa elimu kuhusu usimamizi wa ardhi pamoja na uwepo wa kituo jumuishi kitakachotoa huduma ya kupokea maoni mbalimbali na utoaji hati miliki ,ukadiriaji wa kodi ya ardhi na ulipaji wa kodi ya ardhi.

Gwakisa aliwataka wananchi wa mkoa wa Tanga kuhudhuria na kushiriki ambapo Waziri atakuwepo na wataalamu kutoka Wizarani

Thursday, April 18, 2024

RAIS SAMIA KUFUNGUA MKUTANO WA ALAT 2024 UTAKAOFANYIKA ZANZIBAR

 𝗥𝗔𝗜𝗦 𝗦𝗔𝗠𝗜𝗔 mgeni rasmi Mkutano wa 38 ALAT utakaofanyika Tarehe 23 - 25 April 2024 #Zanzibar

. . #alat @ortamisemi @samia_suluhu_hassan @dr.hmwinyi @jembenijembe @kikotifredy #samiasuluhuhassan #HUSSEINMWINYI #zanzibar

Wednesday, April 17, 2024

SHIRIKA AMEND,JESHI LA POLISI TANGA WAENDELEA KUTOA ELIMU YA USALAMA BARABARANI

 

 


Ofisa Miradi kutoka Amend Tanzania Scholastica Mbilinyi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoa elimu kwa Madereva wa Pikipiki maarufu kama Bodaboda,Bajaji na Madereva wa Daladala katika Stendi ya Pongwe Jijini Tanga
Ofisa Miradi kutoka Amend Tanzania Scholastica Mbilinyi akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutoa elimu kwa Madereva wa Pikipiki maarufu kama Bodaboda,Bajaji na Madereva wa Daladala katika Stendi ya Pongwe Jijini Tanga
Mkuu wa Usalama Barabarani,kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Mrakibu wa Polisi Wiliam Mwamasika
Mkuu wa Usalama Barabarani,kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Mrakibu wa Polisi Wiliam Mwamasika akizungumza na madereva wa bodaboda pikipiki maarufu kama bodaboda,bajaji na daladala






Na Oscar Assenga,TANGA


Shirika la Amend Tanzania kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Tanga chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Switzerland Nchini,wameendesha zoezi la utoaji wa Elimu ya Usalama Barabarani kwa Madereva Daladala na Bodaboda Jiji la Tanga ikiwa ni sehemu ya kupunguza na kutokomeza ajali za barabarani zinazotokana na uzembe wa madereva.

Akizungumza wakati wa utoaji wa Elimu hiyo ya Usalama Barabarani iliyofanyika Aprili 16,2024 katika Stendi ya Pongwe Jijini hapa,Ofisa Miradi kutoka Amend Tanzania Scholastica Mbilinyi, amewaambia waandishi wa habari kuwa lengo ni kuwafikia Madereva 500 na mpaka sasa Madereva 300 tayari wameshafikiwa katika awamu ya kwanza,

Alisema kwamba wamewafikia madereva wa pikipiki maarufu kama (Bodaboda) kuwapa mafunzo ya Usalama Barabarani na waliohitimu wamepewa vyeti huku akieleza wataendelea na kutoa elimu ya usalama barabarani kwa awamu ya pili ambao utaanza mwezi mei mwaka huu na itakuwa endelevu.

Scholastica aliwataka Madereva wa vyombo vyote vya moto kuzingatia sheria za Usalama Barabarani ili kupunguza ajali za barabarani zinazotokana na uzembe wa Madereva,

"Niwaombe Madereva wote hususani wa Bodaboda tuzingatie Usalama Barabarani tusibebe watoto chini ya miaka 9 kwa sababu hawana uwezo wa kuhimili mikikimikiki ya Barabarani na maisha yako ni muhimu zaidi kuliko pesa wanayoitafuta"Alisema


" Tuzingatie Usalama kwanza ili ajali zipungue zibakie zile ambazo haziepukiki ikiwemo kupasuka kwa tairi ,kukatika kwa stelingi au tatizo lolote la kiufundi katika vyombo vyetu vya moto"Alisisitiza Scholastica

Kwa upande wake Mkuu wa Usalama Barabarani,kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Tanga Mrakibu wa Polisi Wiliam Mwamasika aliwataka madereva wote kwenda darasani kama sheria inavyowataka kufanya hivyo,


"Tupo hapa kutekeleza wajibu tuliopewa na Serikali ambayo ni nyie wananchi lakini sote tunafahamu kuwa Serikali mwaka jana ilitoa maelekezo ya madereva wote kwenda kusoma pamoja na kuhakiki leseni zenu,wapo baadhi yenu wametekeleza maagizo ya Serikali"Alisema


Hata hivyo alisisitiza umuhimu wao kuhakikisha wanalitekeleza suala la kusoma huku akiwataka wasifanye jambo kwa shuruti kwa sababu elimu wanayoenda kuipata kwa ajili ya manufaa yao hivyo hawana haja yakulazimishana.

Aidha aliwaonya Madereva wa Daladala kuacha tabia ya kusimamisha Daladala zao kwa muda mrefu kwenye maeneo yasiyokuwa na vituo katikati ya Jiji hili lenye mpangilio mzuri wa namba za Barabara za mitaa,

"Kwa Bahati mbaya wakati wanapangilia Jiji hili walisahau kuweka vituo vingi vya Daladala, hivyo sisi tumeona ni busara tu kwa baadhi ya maeneo kwenye Barabara za namba Daladala inaweza ikasimama kwa muda mfupi sana ili kuepusha msongamano unaoweza kujitokeza,unatakiwa utumie muda mfupi sana kupakia au kushusha abiria wako kwenye vituo tulivyoviruhusu" Alisisitiza SP.Mwamasika

Wednesday, April 10, 2024

VIONGOZI NA WANACHAMA WA CCM KATA YA MSANGANI WAMFAGILIA MWENYEKITI NYAMKA

 


NA VICTOR MASANGU,KIBAHA


BAADHI ya wanachama na viongozi wa chama cha mapinduzi na wananchi wa  Kata ya Msangani wamempongeza kwa dhati Mwenyekiti wa CCM Kibaha mji Mwajuma Nyamka kwa upendo wake wa kuwakutanisha kwa pamoja katika kusherekea sikukuu ya Iddy mosi nyumbani kwake.

Baadhi ya viongozi hao akiwemo Diwani mteule wa kata ya Kata ya Msangani Gunze Yohana ambaye amechaguliwa hivi karibuni kwa kishindo cha asilimia 99.20.

Gunze aliongeza kuwa amefanya jambo la upendo la kuamua kuwakutanisha baadhi ya wanachama,viongozi na wananchi ili kuweza kujumuika katika chakula cha mchana  katika kusherekea sikukuu ya Iddy mosi.

"Kiukweli Mwenyekiti wetu wa chama ameonyesha upendo maana kitendo tu cha kutukutanisha nyumbani kwake  sisi kiukweli tumefarijika na Mungu ambariki kwa moyo wake wa kujitolea ,"alisema Gunze.

Naye balozi wa mtaa wa Kidenge Said Mbunju alisema kwamba Mwenyekiti Nyamka amekuwa mstari wa mbele katika kushirikiana na jamii na kwamba amefarijika sana kushiriki chakula cha mchana nyumbani kwa Mwenyekiti.

"Nafahamu leo hii ni sikukuu lakini sisi tumekuja kwa niaba ya wengine lakini nipende kuchukua fursa hii kumshukuru kwa moyo wangu wote maana tumeweza kukutana na kubadilishana mawazo mbali mbali ",alisema Said.

Mjumbe huyo alisema katika sikukuu watu wengi wamekuwa wakikutana na ndugu zao lakini kwa upendo wa Mwenyekiti akaona akutane na jamii ili kuweza kula chakula cha mchana sambamba na kubadilishana mawazo.

Kwa upande wake Mwenyekiti huyo wa CCM Kibaha mji aliwahimiza viongozi na wanachama wa ccm kuhakikisha wanakuwa na umoja na upendo kipindi chote.

Nyamka alisema kwamba anatambua kwamba katika siku za siku kuu kila mtu anakuwa na majukumu mengi lakini akaona awashirikishe baadhi ya watu ili aweze kujumuika nao katika chakula cha mchana.

 "Mimi kiukweli nawashukuru wale wote ambao baadhi yao niliwaomba tujumuike kwa pamoja na wote mimi ninawapenda japo niliita baadhi tu kwa niaba ya wengine Mungu awabariki sana,"alisema Nyamka.

Kadhalika Nyamka pamoja na kuwapongeza aliwakumbusha viongozi na wana ccm kwa ujumla  umuhimu wa kuhakikisha kwamba wanajipanga vizuri katika kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu na uchaguzi mkuu mwakani.

Mwenyekiti huyo wa CCM Kibaha mji ametumia sikukuu ya Iddy mosi kuwakaribisha baadhi ya viongozi wa ccm,wanachama na wananchi lengo ikiwa ni kula chakula cha mchana pamoja na kubadilishana mawazo.

Barrick yakabidhi msaada wa vifaa vya kisasa vya kupima ulevi wa madereva kwa Jeshi la Polisi

Meneja Mawasiliano (Corporate Communication and Country Liaison Manager) wa Barrick, Georgia Mutagahywa (wa pili kutoka kushoto) akimkabidhi moja ya vifaa vya kisasa vya kupima ulevi kwa madereva vilivyotolewa na Barrick kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama barabarani kanda maalum ya Dar es Salaam, Mohamed Bahashwan, katika hafla ya kukabidhi msaada wa vifaa hivyo kwa Jeshi la Polisi iliyofanyika katika Kituo cha Oysterbay jijini Dar es Salaam , wengine pichani ni Kamanda wa Polisi wa Kinondoni SACP Mtatiro Kitinkwi (kushoto) na Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani wa Dar es Salaam SACP William Mkonda.

Na Mwandishi Wetu.

Katika kuendeleza mkakati wa kuhamasisha jamii kuzingatia usalama wakati wote, kampuni ya Barrick kupitia kampeni yake ya ‘Journey to Zero’ imekabidhi Jeshi la Polisi msaada wa vifaa vya kupima ulevi kwa madereva wa vyombo vya moto vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 100 katika hafla iliyofanyika katika kituo cha polisi cha Oysterbay kilichopo wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Akiongea katika hafla ya kupokea vifaa hivyo,Kamanda wa Polisi wa kanda ya Kinondoni, Kamishna Msaidizi Mwandamizi Mtatiro Kitinkwi,alisema msaada huyo wa vifaa vya kisasa vya kupima kilevi umetolewa kwa wakati mwafaka ambao Jeshi hilo linaendelea na mikakati ya kukomesha vitendo vya ulevi kwa madereva wanaoendesha vyombo vya moto ambao umekuwa ni chanzo kikubwa cha ajali nyingi za barabarani zinazotokea nchini.

“Tunawashukuru Barrick kwa kuendelea kuwa wadau wakuu wa kusaidia kampeni za ualama barabarani nchini na sisi tunawahodi kuwa vifaa hivi tutavitumia vizuri ili vifanikishe lengo lililokusudiwa la udhibiti wa madereva kutumia vinywaji vyenye kilevi kupita kiasi”.alisema Kitinkwi.

Alisema Jeshi la Polisi kupitia kikosi chake cha Ualama Barabarani pia litaendelea kutoa elimu ya unywaji kistaarabu kwa madereva wa vyombo vya moto ili kuhakikisha ajali nyingi zinazotokana na ulevi zinatokomezwa nchini na alitoa wito kwa wadau mbalimbali kuunga mkono jitihada hizi kwa kuwa suala la usalala linamgusa kila mwananchi.

Kwa upande wake Meneja Mawasiliano (Corporate Communications and Country Liaison Manager) wa Barrick, Georgia Mutagahywa, alisema kuwa msaada huo ni mwendelezo wa kampeni ya Barrick ya Journey to zero ambayo inalenga kuhamasisha afya na usalama kwa wafanyakazi wake na wadau wengine wote kwenye jamii.

“Kampeni yetu ya 'Journey to Zero' inalenga kuhakikisha wafanykazi wote wa kampuni wanakuwa salama wakati wote wanapokuwa kazini hadi wanaporudi nyumbani hivyo tumehakikisha kampeni hii inavuka mipaka hadi nje ya kampuni kuhakikisha jamii nzima inakuwa salama na ndio maana tunaendelea kuunga mkono Serikali kupitia Jeshi la Polisi kupambana na changamoto ya ajali za barabarani.

Mutagahywa alisema Barrick, siku zote itaendelea kuwa mstari wa mbele kushirikiana na wadau mbalimbali kuunga mkono kampeni hizi za usalama barabarani na inaamini vifaa hivi vya kisasa vya kupima kilevi vilivyokabidhiwa kwa Jeshi la Polisi vitasaidia kuwabaini madereva wanaoendesha vyombo vya moto wakiwa wamelewa na kuchukuliwa hatua za kisheria ili kudhibiti na kupunguza matukio ya ajali za barabarani.

Naye Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Kamati za Usalama barabarani nchini, Idd Azzan, aliishukuru Barrick, kwa kutoa msaada huo na kwa kuwa mdau mkuu wa kusaidia kampeni ya usalama , alitoa rai kwa watumiaji wa vifaa hivyo kuvitunza vizuri ili kuweza kufanikisha malengo mazuri yaliyokusudiwa sambamba na kuwarahisishia kazi, “Katika dunia ya sasa ya matumizi ya teknolojia nina imani vifaa hivi vitarahisisha kazi ya polisi wetu kuwanasa madereva walevi” alisisitiza.
Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Kamati za Usalama barabarani nchini, Idd Azzan akiongea katika hafla hiyo.
Maofisa mbalimbali waandamizi wa Jeshi la Polisi wakifuatilia matukio katika hafla hiyo
Maofisa mbalimbali waandamizi wa Jeshi la Polisi walipata fursa ya kuongea katika hafla hiyo.
Viongozi wa kamati za usalama barabarani, Jeshi la Polisi na Barrick walipata fursa ya kupiga picha ya pamoja na wageni waliohudhuria katika hafla hiyo.

RC BATILDA –TANGA TUMEPOKEA ZAIDI YA TRILIONI 2 ZA MIRADI YA MAENDELEO

 

 


MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian akiwa kwenye futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Waziri wa Maji 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhamani akizungumza katika halfa hiyo 
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akitunzwa baada ya kusoma Quarn Tukufu katika halfa hiyo 




Na Oscar Assenga, PANGANI.

MKUU wa Mkoa wa Tanga Balozi Batilda Burian amesema katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt Samia Suluhu mkoa huo umepokea fedha kiasi cha Sh.Trilioni 2.6 kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Balozi Batilda aliyasema hayo wakati wa Dua Maalumu ya Kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu iliyokwenda sambamba na Futari iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Pangani (CCM) na Waziri wa Maji Jumaa Aweso iliyofanyika wilayani Pangani.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa Serikali,Chama na Taasisi mbalimbali akiwemo Naibu Waziri wa maji Mhandisi Mathew Kundo, Katibu Mkuu Wizara ya Maji,Mkurugenzi wa Ruwasa na wataalamu mwengine.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema fedha hizo zimeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo likiwemo Daraja la Mto Pangani na Barabara ya Pangani pamoja na mengine ikiwemo ya elimu ambapo wanamshukuru Rais kwa ujenzi wa mabweni ya watoto wenye mahitaji maalumu yamejengwa,zahanati,nyumba za walimu na miradi ipo mingi kazi kubwa imefanywa.

“Katika hili tunamshukuru sana Mh Rais Dkt Samia Suluhu kwa kutuletea fedha hizi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo lakini namshukuru kwa imani kubwa kwangu ninahaidi sitamuangusha nitajitahidi kwa ushirikiano wenu na dua zengu niweze kutimiza yale ambayo anakusudia nitimize nikiwa hapa Tanga”Alisema RC Balozi Batilda

Alisema kwamba wataendelea kuhakkikisha fedha zinazokuja zinatekeleza kazi iliyokusudiwa na sio vyenginevyo pamoja na usimamizi mzuri katika miradi inayotekeleza ili iweze kuleta tija inayotakiwa.

“Nimshukuru Waziri Aweso amefanya jambo kubwa na ameendelea kufanya mambo mengi kwenye Sekta ya Maji nimetoka Tabora kwenye miradi 28 nasi tulikuwa tunanufaika nimekuja hapa Tanga nimeambiwa napo ipo ni kijana mdogo lakini mwenye hekima,hofu ya mungu ,mchapakazi “Alisema RC Balozi Batilda.

Alisema kwa hakika dhamana aliyopewa na Rais Dkt Samia Suluhu kuhakikisha anawatua wakina mama ndoo kichwani ameitekeleza vizuri kwa kushirikiana na wataalamu wa wizara maji wanaendelea na kazi nzuri.

Akizungumzia suala la mabadiliko ya tabia ya nchi hasa kwenye wilaya ya Pangani RC Balozi Batilda alisema wilaya hiyo ni moja ya maeneo yaliyoathirika na kuna maeneo yakichimbwa visima kuna maji ya chumvi ndio maana kwenye mradi wa maji ya miji 28 na wao wamepelekewa na maeneo watachimba visima ili wananchi waweze kunufaika kwa kupata maji safi na salama.

Akizungumzia suala la uvuvi RC huyo alisema suala hilo katika mkoa huo ni moja ya maeneo ya uvuvi hivyo suala la maboti na vifaa vya uvuvi vitaendelea kupatikana kwenye mji wa Pangani na maeneo mengine.

“Tunapozungumzia masuala ya mazingira niwape kongole Pangani mazingira mmeendelea kuyatuza na msitu wenu wa asili unapendeleza”Alisema

Mkuu huyo wa mkoa alisema katika moja ya kuendeleza ukwekezaji Serikali kupitia Wizara Madini ilisaini mkataba na wawekezaji wa madini ya Ndovu au tembo ambayo yatachimbwa kwenye Mwambao wa Pangani karibu kilomita 15 ya ufukwe.

Alisema walichowaambia wahakikisha hawawanyi ruhusu ya wavuvi kutumia mwambao huo na matumbawe hayatavurugwa ikiwemo mikoko iliyopo wakati wanaendelea kunufaika na mradi huo na kuendelea na uvuvi,matango pori yote kuhakikisha wanakuwa na shughuli mbalimbali zinaendelea.

Hata hivyo Mkuu huyo wa mkoa alisema mkoa wa Tanga ndio ambao kila kitu kinaweza kuota hivyo lazima wahakikishe utajiri huo unawanufaisha wananchi wao wote kwa kuhakikisha wanachangamkia fursa zilizopo.

“Katika ujenzi wa bomba la mafuta litapita kwenye wilaya kadhaa tunataka wana tanga wanufaike na miradi hiyo na kazi yake katiba tawala na wakuu wa wilaya na makatibu tawala ni kuwawezesha wananchu kuona fursa za uwepo wa mradi huo ili waweze kuchangamkia fursa hizo”Alisema RC Balozi Batilda ,

Awali akizungumza katika futari hiyo Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew alisema kwamba maadili mema ambayo tumeyaonyesha katika kipindi cha mwezi mtukufu wa ramadhani tuendelee kuifanya na kufanya ibada ndio tunaweza kuwaponya wengi na kujiponya na sisi.

Mhandisi Mathew alisema pia waendelee kumuombea Rais Dkt Samia Suluhu ili aendelea kuifanya kazi nzuri anaoendelea kuifanya na kuhakikisha wanashirikiana na Mbunge wao na kamwe wasimwangushe .

“Nataka kuwaambie wana Pangani “Dhahabu ya Pangani tunaijua wana Pangani na Dhahabu ya Tanzania tunaijua na tusije kudanganyika na kuachia dharabu hii na kwenda kuokota mawe”Alisema

Hata hivyo alimshukuru Waziri Aweso kwa jambo kubwa alilolifanya kwa wananchi wake kutokana na uwepo wa umoja na mshikamano kwa wananchi wake ambao wameitika kwa wingi kwenye tukio hilo.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman alisema safari ya kuifungua pangani kimaendeleo itafanywa na wana Pangani wenyewe na mimi ni miongoni mwa watu walishawishika na Waziri Aweso kipindi kile kwa maneno yake kwa dhamira iliyojificha ndani ya moyo wake akanitamkia ya kutaka kuwatumikia wananchi wa Jimbo hilo.

Alisema kwa sasa tunayaona maendeleo makubwa sana kwenye Jimbo la Pangani ikiwemo ujenzi wa barabara ya Tanga-Pangani –Saadani ambayo itaifungua wilaya hiyo pamoja na uwepo wa miradi ya maji ambayo awali wananchi walikuwa wakiifuata umbali mrefu.